Hapo zamani za kale kulikuwa  na mfalme. Katika kijiji cha mfalme kulikuwa na mtu na mkewe ambao walipendana sana. Siku moja mtu huyu alienda safari.

Baada ya mtu huyu kuondoka, mfalme alianza kufanya ziara katika kijiji chake. Alipokuwa akipitia karibu na nyumba ya mtu huyo aliona bibi ya mtu huyo na akapendezwa sana na sura yake.

Aliporudi kwake nyumbani alituma mtumishi wake aende akamwambie bibi huyo kuwa anampenda sana na angeenda kumtembelea.

Bibi huyo alirudisha ujumbe kwamba yeye alikuwa na bwanake ambae alimpenda sana.

Hata baada ya kupewa ujumbe huo mfalme huyo hakukata tamaa. Alituma mtumishi wake arudi akamwambie yule bibi kuwa angeenda kumtembelea.

Alipoenda kumtembelea huyo bibi kulikuwa usiku. Mfa;me alikuta bibi huyo tayari. Alikaribishwa vyema na akaandaliwa chakula. Chakula alichoandaliwa kilikuwa na rangi tatu tofauti. Baada ya kumaliza chakula hicho, bibi huyo alimuuliza mfalme

Chakula hicho kilikuwaje?

Mfalme akajibu,
“Hata ingawa chakula
hicho kilikuwa na rangi
tatu tofauti,
ladha yake ilikuwa moja.”

Bibi huyo akajibu

“Vivyo hivyo ndivyo
wanawake walivyo.
wana sura mbalimbali
lakini ladha yao ni moja.”

Bibi huyo aliendelea kumwambia mfalme kuwa atulie na aache kumsumbua kwa vile yeye alikuwa na bwanake.

Mfalme akaona aibu na akatoka mbio na katika mbio hizi akaacha kiatu  chake.
Mume wa bibi huyo aliporudi alikuta kiatu cha mfalme kwake na akashangaa sana.
Alijiuliza

“Mfalme alikujaje kwangu?”

Aliamua kuwa ni lazima pawe na uhusiano kati ya mkewe na mfalme. Aliamua kumwacha mkewe.

Mkewe alipoona kuwa mumewe hakuwa na haja naye, alienda kumshitaki kwa mfalme. alimsimulia kisa cha mtu ambaye alikuwa na shamba. Alikuwa anapalilia shamba lake kwa  juhudi na uangalifu wa hali ya juu.

Shamba hilo lilikuwa na matunda,
waua, miti na kila kitu. Watu
walikutwa wanapendezwa na shamba hilo
lakini sasa mtu huyo amelitupa shamba hilo
lake. Halijali tena. Halimi na matunda
na mazao mengine hayapatikani tena.

Mfalme alielewa ujumbe uliokusudiwa na huyo bibi
kutokana na kisa hicho. Aliita mtumishi wake
na akamtuma akamwite bwana wa bibi huyo.

Bwana wa bibi huyo aliitika wito wa mfalme
na akaenda. Alipofika huko, alipewa mashtaka
ambayo yalikuwa yametolewa na mkewe.

Aliyakubali lakini akajitetea. Alisema kuwa alitupa shamba lake tu baada ya kuona wayo la shamba ambaye alikuwa akupitia shambani mwake. Aliona ni hatari kuendelea kulima shamba hilo na akaogoppa na akamua kuliacha asije akahatarisha maisha yake.

Mfalme alielewa utetezi wa bwana huyo ……. Alimweleza kuwa ni kweli kuwa simba alikuwa amepitia shambani mwake lakini hakugusa chochote. Kwa hivyo mfalme alimuhimiza yule bwana arudi akapalilie shamba lake kama alivyokuwa akifanya hapo awali.

(Jibu maswali yafuatayokutokana na hadithi hii)

(1) Eleza maudhui muhimu ambayo yanajitokeza katika hadithi hii
(2) Bainisha dhamira kuu na dhamira ndogo amazo zinapatikana katika hadithi hii.
(3) Msanii ametumia mbinu zipi katika kuwasilisha maudhui yake?

Katika hadithi hii ujumbe tunaoupata ni kwamba ugomvi waweza kutokea kwa sababu ya mambo yasiyo na msingi. Kwa mfano tunaonyeshwa jinsi mfalme alivyoelimishwa kuhusu uchu wake na kuonyeshwa kwa fumbo la chakula kuwa hata ingawa wanawake hujitokeza kwa sura mbalimbali wote ni kitu kimoja na ladha zao ni sawa.

Vile vile tunaonyeshwa jinsi ugomvi unavyoweza kuzuka baina ya mtu na mkewekwa sababu ya ukosefu wa mawasiliano. Kama kungekuwa na uelewano bibi angalimueleza mumewe kuhusu safari ya mfalme nyumbani jwao na yale yaliyotendeka. Mawasiliano hayo yangezuia mashtaka waliopeleka kwa mfalme ambaye ndiye alikuwa chanzo cha mgogoro wao.