May 30, 2016
Katika hali isiyotegemewa na Watanzania wengi, Naibu Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson amesitisha kusikilizwa kwa hati ya dharula ya kujadili kufukuzwa kwa wanafunzi 7,802 wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambao walipewa masaa 24 kuondoka chuoni.
Akielezea sababu ya kurudishwa nyumbani kwa wanafunzi hao waliokuwa wanachukua Diploma ya Ualimu Sayansi, Waziri wa Elimu, Dk. Joyce Ndalichako amesema sababu ni kugoma kwa walimu kuwafundisha sababu yakiwa ni madai yao kwa uongozi wa chuo.
“Sisi kama serikali hatuwezi kuingilia madai yao ni mambo ya hesabu za ndani tunachokifanya ni kusuluhisha ili walimu waendelee kundisha
“Kutokana na kuona bado kuna mgogoro kwa walimu na chuo tumeona ni vyema kuwarudisha nyumbani wanafunzi 7,802 wakati serikali inaendelea kufanya jitihada za kumaliza mgogoro uliopo na baada ya kukamilika wataendeleea na masomo,” amesema Dkt. Ndalichako.
Baada ya hapo mbunge wa Arumeru Mashariki, Mh. Joshua Nassari alimwomba Naibu Spika, Dkt. Tulia Ackson kutoa muda ili waweze kujadili hati hiyo ya dharula iliyotolewa na Mbunge wa Chemba, Mh. Juma Nkamia jambo ambalo Naibu Spika alisema siyo dharula na hivyo wabunge wa vyama vyote kwa pamoja kuungana na kutoka nje ya bunge.
Akizungumza baada ya kutoka nje ya bunge, Mbunge wa Bunda Mjini, Mh. Ester Bulaya amesema jambo pekee wanalohitaji kwa sasa ni bunge kutenga muda wa kujadili jambo hilo ambalo linaonekana kuwa na umuhimu zaidi kwa sasa.
“Hapa tunajadili mambo ya nchi na sasa kuna wanafunzi wengi wamesamba mjini hawana sehemu za kwenda alafu naibu spika anasema sio dharula tunachohitaji ni kujadili jinsi gani tunawasaidia wanafunzi hawa,
“Niwapongeze wabunge wa CCM leo kwa mara ya kwanza wamekubali kuungana na upinzani na kutoka nje ya bunge wakihitaji kujadiliwa hatma ya wanafunzi zaidi ya 7,000 wa UDOM ambao hawana sehemu ya kwenda,” amesema Bulaya.
Leadingg News and Events
-
Soma tangazo lililotumwa kwa vyuo vinavyotoa mafunzo ya ualimu vinavyotambuliwa na serikali.
-
Our Current Domain Prices Visit this page often, we usually have promotions on domains every once in a while on variou...
-
HI 368, Oral Histories in Tanzania: Theory Topic 1: Basic definitions and identification of typologies • Definition of terms CULTURE...
-
So when you have sex before marriage you’re playing with fire that will most certainly burn you at some point in your life… especially in y...
-
Hapo zamani za kale kulikuwa na mfalme. Katika kijiji cha mfalme kulikuwa na mtu na mkewe ambao walipendana sana. Siku moja mtu huyu alien...
-
Katika hali isiyotegemewa na Watanzania wengi, Naibu Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson amesitisha kusikili...
-
Job Vacancy > Office Attendant-Iringa Location > Iringa Position Type > Full Time Organization Type > Company Mwanan...
-
This study focused on the impacts of challenges facing teachers on curriculum implementation in Nyamagana District. The study involve...
-
To be pure,to remain pure, can only come at a price, the price of knowing God and of loving him enough to do his will. He will always gi...
-
The object of marriage is to glorify God by serving one's spouse and helping the spouse reach his or her God-given potential! ...